Msalaba, ni moja ya kitu
aua alama ambayo niya maana sana katika maisha ya wakristo wengi, uwezi
kuongelea injiri pasipo kutaja msalaba ambao Bwana Yesu aliuwawa juu yake. Kwa
zaidi ya miaka elfu mbili sasa msalaba umekuwa na uhusiano mkubwa sana kanisa kwa
maana wakristo. Msalaba umekuwa kiwakilishi cha wokovu, ushindi, rehema,
tumaini pia umekuwa ishara ya Yesu Kristo na pia kanisa maana watu waonapo
msalaba umechorwa mahali popote ujua kuwa mahali hapo kuna mkristo au ukristo,
wakristo wametumia alama za misaraba katika makanisa, nyuma zao kuonyesha au
kukili mbele za watu juu ya Imani yao, wengine wamevaa shingoni na hata wengine
kuchora katika mavazi yao. Hakika msaraba umekuwa na uhusiano na muunganiko
mkubwa na maisha yetu pia na mwokozi wetu Yesu Kristo.
Lakini kabla ya Bwana Yesu kusurubiwa na kufufuka msalaba haukuwa na maana nzuri kwa mwanadamu yeyote kama leo hii, ulitisha na kuogopwa na wote na hakuna mtu ambaye alitaka kujihusisha nao kabisa.
Lakini kabla ya Bwana Yesu kusurubiwa na kufufuka msalaba haukuwa na maana nzuri kwa mwanadamu yeyote kama leo hii, ulitisha na kuogopwa na wote na hakuna mtu ambaye alitaka kujihusisha nao kabisa.
KIFAA CHA MATESO
Msaraba hapo zamani ulikuwa
ni kifaa kilichotumika kutesea watu kabla ya kufa, mtu alitundikwa msarabani
akiwa hai na kugongelewa misumari mitatu pekee kwenye viganja viwiri vya mikono
na miguu ukusanywa na kugongelewa pamoja, hakika yalikuwa mateso sana kwanza
ile misumari uliyogongelewa pia ni pale ukisimamwishwa maana mwili mzima ubebwa
na misumari mitatu mikubwa iliyokuwa mikononi na