ETI YESU NI VALENTINE WAKO?? HIVI UNAJUA UNALOSEMA??
![]() |
| Picha ya aitwaye Valentine aliyekuwa |
Maana kama kigezo ni hicho tu kwamba sio ya Kikristo, swali
moja najiuliza; hapa Tanzania tuna sherehe za Muungano, Uhuru na Mapinduzi,
tuna zingine kama MEI MOSI, na zinginezo ikiwemo NYERERE DAY, sioni kama hizo
ni za Kikristo, lakini mbona wanashiriki?
Mimi nadhani kuna haja ya kurudi nyuma na kuchunguza
historia ya namna hii siku ilianzishwa, na nini malengo yake ya kuadhimishwa.
Mimi nilijipa muda huo tangu siku za nyuma, nimekuwa nikieleza maoni yangu sio
leo tu, na hapa nitaeleza tena kidogo.
ASILI YA NENO VALENTINE
Neno Valentine linatokana na jina la jamaa mmoja wa
Kikatoliki (leo tungesema alikuwa Padri) ambaye aliishi kwenye mji wa Roma huko
Italy, alikuwa anaitwa VALENTINE au kwa Kiswahili Valentino. Aliishi enzi za
utawala wa Claudius (Claudio).
Nitakueleza ilikuwaje siku hii ikaitwa jina lake. Kuna dhana
nyingi kuhusu siku hii, lakini ziko mbili zenye mashiko, kwangu mimi zote
hazina uhusiano na UPENDO au UKRISTO bali mahaba au hisia za kimapenzi.
Nitafafanua!
Katika kulifanya jeshi lake liwajibike katika vita, Mfalme
Claudio aliwapiga marufuku Wanajeshi wake kuoa, lakini pamoja na marufuku hiyo
huyu Padri Valentino aliendelea kufungisha ndoa za wanajeshi waliokuwa wanataka
kuoa wakati mwingine pengine kwa siri.
Jambo hili lilipogundulika kwa Mfalme Claudio Valentino
alifungwa gerezani.
Akiwa Gerezani huyu jamaa ‘akajikuta’ anampenda binti mmoja wa
Mfanyakazi wa gereza alilokuwa amefungwa. Nataka nisisitize hapa, kwamba
alimpenda binti huyu ambaye hakuwa dada yake, wala mama yake, wala mpwa wake,
wala mjukuu wake, wala uhusiano wowote wa damu, bali alimpenda KIMAHABA/HISIA
ZA KIMAPENZI. Uzuri hapa ninyi wote ni watu wazima, mtakuwa mnanielewa
ninachomaanisha!
![]() |
| Padri Valentine akifungisha ndoa ya askari |
Ifahamike pia kwamba wakati huo kulikuwa na siku kuu fulani
ya kipagani ambayo iliadhimishwa kipagani, siku kuu hii iliitwa LUPERCALIA
ambayo ilikuwa ikisheherekewa mnamo tarehe 15 februari. Lakini wasichojua wengi
ni kwamba huyu LUPERCALIA alikuwa ni mungu wa kiroma, walimwamini katika
masuala ya kilimo.
Baada ya Valentino kufa, siku hii ya LUPERCALIA mungu wa
kipagano ikabadilishwa jina kwa heshima ya Valentino na kuitwa siku ya
valentine au VALENTINE DAY. Hivi kweli Mkristo hujashtuka tu mpaka hapo?
SWALI NA ANGALIZO
![]() |
Kimazabau cha kufanya maombi kwa
MtakatifuValentino
na sanamu yake
|
Ukiondoa hilo, leo hii kuna watu wanatumia Valentine Day
kuwatumia mama zao, baba zao kadi nk, je, hii ndio asili yake? Kama sheria za
ulimwengu wa roho zinafanya kazi, usalama wetu uko wapi mtoto wa kike anaposema
baba yake mzazi ndiye Valentine wake? Au watu bila haya wanapoandika kwenye
facebook eti Yesu ni Valentine wake?
Nini kinaendelea kwenye ulimwengu wa roho? Sijakataza mtu,
nimeweka maswali ambayo na mimi pia najiuliza, kama ni kujibu wote tusaidiane,
lakini kumwita dada yangu wa tumbo moja au washirika wangu kanisani Valentine,
duuh!! Inaleta KIGUGUMIZI hasa nikizingatia neno Upendo alilolitumia Valentine siku ile! NAWAPENDA!
![]() |
Mtakatifu Valentino wa Katoriki akipokea lozari
toka kwa Bikira Mariamu.
|




Kweli mwalimu haistahili kwa mkristo kusherehekea hii siku.0756201989 & 0719386301.nitumie hata message mi ntakupigia nna shida na we mwalimu.ni Mimi Allan Joseph at Mganyizi
ReplyDelete