Tunaposoma Biblia tunaona Mungu
mara nyingi akisema na watu kupitia ndoto wawapo wamelala kama vile Ibrahimu,
Yakobo, Yusufu, Suleimani, Yusufu (baba wa Yesu), Petro n.k Na bado mpaka leo Mungu anaendelea kusema na
watu kupitia ndoto lakini baadhi ya watu upuuza ndoto kwa kkuto kujua ndoto ni
kitu gani katika maisha ya kiroho.
Kimsingi ndoto ni picha za matukio
1. KUSHIKA SHERIA ZA MUNGU
Sheria za Mungu
ni Neno lake, ili uweze kutunza ndoto yako na kuifanya itimie sawa na Mungu
alivyopanga na wakati usika ni vizuri kusoma Neno la Mungu na kulitimiza kama
lisemavyo. Unapoona umeenda nje ya Neno la Mungu na kutenda dhambi geuka mara
moja na utubu na kumwomba Mungu akaupe nguvu za kushika sharia yake na
songambele.
![]() |
| Ndoto ni kama mshumaa uwakao, unahitaji kutunzwa usije kuzimwa na upepo uvumao wa adui Shetani na wakala wake. |
2. KUISHI MAISHA YA MAOMBI
Watu wengine kwa
kuwa wanajua ndoto ni bayana na hakika zitokee hivyo wakiota tu ndoto uacha
kuomba na kusema zitatokea bila kujua maombi pia uhitajika kutengeneza njia ya
kuelekea kwenye ndoto yako kwa mda usika. Lazima kama mkristo kishi maisha ya
kushindana na kujua wakati wote kunapotokea jambo la kimungu basi Shetani naye
ujiinua hivyo unapoota ndoto njema ya kimungu tambua Shetani naye anajiandaa
kuzuia isitokee hivyo kaa katika maombi daima mpaka iweze kutimia.
3. KUWA MWAMINIFU KATIKA KUMTOLEA MUNGU.
Kumtolea Mungu
siyo ombi bali ni sheria na kanuni moja wapo ya msingi kwa kila mtu wa
Mungu, katika kumtolea Mungu kuna baraka,
lakini kwa hasiyemtolea kuna laana hivyo ni vizuri kutambua utoaji wa sadaka
kama fungu la kumi (zaka) na sadaka nyengine ni muhimu sana. Mungu alisema
katika kitabu cha Malaki kuwa unapomtolea Zaka yeye atakemea yule alaye,
anaposema yule alaye anamaanisha kuna mashetani ambao uweza kutengeneza matukio
au vitu ilikutafuna mapato yako kama vile magonjwa, majanga, kesi na mengine
mengi, unakuta mtu Mungu amekuonyesha katika ndoto utapata cheo fulani kazini
na unapokalibia kupata kwa kuwa haukuwa mwaminifu na sharia ya Mungu inasema
lazima umtolee sadaka na unakuta wewe haumtolei hivyo yeye alaye anakuja kwa
mfano wa kesi ya uongo kazini na unaonekana kuna fedha uliiba na watu wanaanza
kuamini ni kweli na kumbe siyo na kukuta unakosa uaminifu kwa bosi na anaacha
kukupandisha ngazi na unabaki pale pale na kushangaa na kuanza kuona mbona
uliota unapanda na haujapanda kumbe ni kule kuto kumtolea Mungu.
4. KUWA MWAMINIFU KWA MUNGU KATIKA KAZI ZAKE
Ni vizuri kuwa
mwaminifu katika kazi zake, kazi za Mungu ni nyingi siyo kuhubiri au kuimba
bali hata kushuhudia watu Neno la Mungu, kuwaombea watu wanapopatwa na shida
kwawao kujua au kuto kujua, kusaidia watu wenye uhitaji, kufanya usafi
kanisani, kualika watu wa kazini, mtaani au sehemu mbalimbali kanisani n.k Kazi
za Mungu ni shughuli zote au vitu vyote ambavyo ukifanya vinamrudishia Mungu
utukufu na heshima na unapokuwa mwaminifu kwa maana ya kujitoa na kujituma,
kufanya kwa kumaanisha siyo kwa unyonge au kulazimishwa na mtu, kuto kuona aibu
ufanyapo n.k Kwa kufanya hivi unamfanya Mungu kujishugulisha na mambo yako na
kukufanikisha.
5. KUISHI VIZURI NA WATU
Mungu usaidia
watu, ubariki watu, uponya watu n.k lakini kupitia watu. Mungu anapotaka
kumbariki mtu utumia watu, Mungu hawezi kukushushia fedha chumbani kwako ila
anaweza kukupatia wazo na kuanza biashara na katika biashara akakuletea watu
ambao wakanunua bizaa zako na kuziongelea vizuri na kukuletea fedha ambazo
zikawa baraka hivyo ni vizuri kuwatendea watu vizuri kwa kuwa hao hao utumiwa
na Mungu siku ya mwisho, kama utaishi nao vibaya itakapofika wakati wa watu
kutumiwa ili kufanikisha ndoto yako watu hao watakuwa hawawezi kutumiwa maana
wameumizwa na wewe kwa kuwatukana, kuwasema vibaya, kuwadharau n.k hivyo
hawataweza kukujia, unapoishi na ndugu au jirani vizuri ni rahiisi Mungu kusema
nao juu ya wewe na wakakusaidia. Jambo jengine ni kuwa Mungu anapenda watu sana
na ukitaka kujua kiwango cha upendo wake ni kule kujifanya mwanadamu na kufa
msalabani kwaajili yao, hivyo unapoishi vizuri na watu na kuwasaidia unampendezesha
Mungu maana wanadamu anawapenda sana na unapojihusisha na watu wake nay eye anajihusisha
na wewe.
6. KUWA MSIRI
Unapoota ndoto
au kuwa na ndoto kila mtu siyo wa kumwambia ndoto yako maana wengine ni adui,
tunaona Yusufu aliwaambia ndugu zake na hao hao wakata kumuua kwa kumwonea wivu
juu ya ndoto zake, ni vizuri unapoota ndoto au kuwa na ndoto usimwambie kila
mtu, kuwa makini maana siyo kila ndoto ya watu kujua maana ndoto nyingine niza
wewe pekee kujua na siyo wengine. Kabla ya kumshirikisha mtu ndoto yako,
jiulize je Mungu ameniruhusu kuwaambia watu na ukijua hajakuruhusu au kukuambia
acha mara moja usije kuwaambia watu wakaanza kushindana na ndoto zako au
kufanya vita na wewe kwa wazi au sirini na mwisho kuichelewesha ndoto yako.
Kutunza siri pia ni moja ya sifa ya Mungu na watu wa Mungu pia.
Kama mkristo ni
vizuri kuyajua haya na kufanyia kazi ili kuishi na kufika pale Mungu ametaka
ufike.

No comments:
Post a Comment