Friday, 14 October 2016

MSARABA



Msalaba, ni moja ya kitu aua alama ambayo niya maana sana katika maisha ya wakristo wengi, uwezi kuongelea injiri pasipo kutaja msalaba ambao Bwana Yesu aliuwawa juu yake. Kwa zaidi ya miaka elfu mbili sasa msalaba umekuwa na uhusiano mkubwa sana kanisa kwa maana wakristo. Msalaba umekuwa kiwakilishi cha wokovu, ushindi, rehema, tumaini pia umekuwa ishara ya Yesu Kristo na pia kanisa maana watu waonapo msalaba umechorwa mahali popote ujua kuwa mahali hapo kuna mkristo au ukristo, wakristo wametumia alama za misaraba katika makanisa, nyuma zao kuonyesha au kukili mbele za watu juu ya Imani yao, wengine wamevaa shingoni na hata wengine kuchora katika mavazi yao. Hakika msaraba umekuwa na uhusiano na muunganiko mkubwa na maisha yetu pia na mwokozi wetu Yesu Kristo. 

 Lakini kabla ya Bwana Yesu kusurubiwa na kufufuka msalaba haukuwa na maana nzuri kwa mwanadamu yeyote kama leo hii, ulitisha na kuogopwa na wote na hakuna mtu  ambaye alitaka kujihusisha nao kabisa.

Askari wa kirumi wakitundika watu misarabani pembezoni
mwa njia.
                                                                                                                                                                                                                                
KIFAA CHA MATESO
Msaraba hapo zamani ulikuwa ni kifaa kilichotumika kutesea watu kabla ya kufa, mtu alitundikwa msarabani akiwa hai na kugongelewa misumari mitatu pekee kwenye viganja viwiri vya mikono na miguu ukusanywa na kugongelewa pamoja, hakika yalikuwa mateso sana kwanza ile misumari uliyogongelewa pia ni pale ukisimamwishwa maana mwili mzima ubebwa na misumari mitatu mikubwa iliyokuwa mikononi na
miguuni, hakika ni maumivu makali sana.

KIFAA CHA KUAIBISHA

   Msaraba ulitumika pia kumwaibisha mtu, kila aliyetundikwa msarabani sharti alitundikwa akiwa uchi na msaraba ulikuwa ukiwekwa maeneo yenye kusanyiko la watu na hasa katika milango ya kuingilia mjini ili kufanya watu wote wanaoingia na kutoka mjini kuweza kukuona wazi kitu ambacho ni aibu kubwa.

KIFAA CHA KUTISHA WATU

Miili ya watu ikiwa imeachwa msarabani.
    Msaraba ulitumika kutisha watu juu ya serikali na tawala fulani, mfano utawala wa Warumi ulikuwa ukitumia msaraba katika makoloni yao kusurubisha na kuulia waarifu wote wa serikali kwanzia wale wasiotii amri ya utawala wao wa kikoloni au kutaka kusimama kinyume chao hivyo walitundikwa wakiwa wamepigwa sana na kuumizwa pembezoni wa njia na milango ya kuingia mjini huku juu ya msaraba wakiweka kibao chenye kuonyesha kosa la mtu na wakati mwingine utundika kile alichoiba kama kinatundikika lengo kuu kila mtu anayeingia katika mji aogope utawala wao na aelewe kuwa anapaswa kufuata sheria za warumi aingiapo katika miji yao na wanaotoka ni ili waweze kwenda kuwaambia watu juu ya warumi.

 KIHASHIRIA CHA LAANA

Biblia inakili kuwa kila ambaye ametundikwa msarabani amelaaniwa na kwa sheria za wayahudi ambazo walipewa na Mungu pia ni pale anapotokea mtu akatenda kosa la kustahili kifo ambalo ni laana basi atundikwe msalabani ila usiku usifike mwili wake bado ukiwa unaninginia msarabani bali ashushwe maana wasipofanya hivyo Mungu alisema laana ya mtu huyo inakuwa juu ya nchi japo kwa warumi haikuwa hivyo wao mwili wa mtu ulikaa hata zaidi ya siku moja ili kutoa fundisho na onyo kwa watu kuto kutenda kosa kama alilotenda huyo aliyeuawa. Hivyo tunaona msaraba ulikuwa ishara ya laana.

KIFAA CHA KIFO
Lakini zaidi ya yote msaraba ulitumika kama kifaa cha kuulia mtu, watu ambao walihukumiwa kifi hasa kifo cha aibu, maumivu na mateso basi msaraba ulikuwa ndiyo kazi yake kwa kuwa mtu hakufa haraka bali alikuwa akifa kidogo kidogo ila kwa maumivu na uchungu mkali sana, damu ilitulilika kidogo kidogo mpaka pale mwili ulipoishiwa na damu na kushindwa kufanya kazi yake vizuri ndipo mtu ufa. 

BWANA YESU NA MSARABA
Msaraba, kimbilio la mataifa.
Mafarisayo, Masadukayo na Wayahudi walitaka Bwana Yesu auawe kifo cha mateso, uchungu na aibu kuu mbele za watu wote na kuwa onyo kwa wafuasi wake na kuwatisha wasiendelee na mafundisho ya Yesu na kuonya wengine wasije kufanya kama Yesu na njia pekee ya kutimiza hayo waliweza kuona ni msaraba na siyo upanga kama kwa Yohana Mbatizaji, Mawe kwa Stefano ila msaraba. Mauti ya Yesu msarabani ilikuwa ni mauti ya uchungu, aibu na maumivu.

Baada ya kupigwa sana mijeredi thelathini kasolo mmoja na askari wa kirumi aliweza kupewa adhabu ya kwanza ya kuubeba msaraba wake kwenda nao nje ya mji mahali paitwapo Goligotha yaani fuvu la kichwa, aliubeba akiwa kachoka na mwenye maumivu makali sana na kuanza kupita katika kinjia chembamba sana chenye kusheheni watu wengi wenye kumsonga pande zote wengine wakimtukana, wengine wakimtupia mawe huku askari wa kirumi wakimzingira kuhakikisha anafanikiwa kufikisha msaraba wake sehemu husika na kweli alifanikia kufika na huko alikutana na waarifu wawili ambao nao walihukumiwa kifo cha aibu na maumivu cha msaraba. 

Hakika inasikitisha sana. Akiwa Goligotha alivuliwa nguo na kuwa uchi kisha kugongelewa msarabani na kusimamishwa na msaraba kutoka saa sita mchana mpaka saa tisa alasiri alipodai kusikia kiu na akapewa siki yenye uchungu mkali, ndipo sasa akapaza sauti yake akimwisema IMEKWISHAAA na akaitoa Roho yake ndipo nchi ilipotikisika na misingi yake huku makaburi yakifunguka na miili mingi ya watu ikitokeza ndani yake na kuingia mjini.
Baada ya siku tatu Bwana Yesu yu hai, hakika yu hai milele.
 
MAANA MPYA YA MSARABA
Ukitaka kujua kuwa Yesu Kristo alikuwa na nguvu ya ajabu ya kubadilisha uovu kuwa wema, giza kuwa nuru, uzuni kuwa furaha, kilio kuwa kicheko, usiku kuwa asubuhi utaweza kuona kwanza katika msaraba.

Msaraba hule hule ambao ulikuwa ni kifaa cha kuaibisha, kutesa, kuua, kuuzunisha na ishara ya laana, kifo n.k ameweza kuibadili kwa kifo chake na kufanya leo hii msaraba kuwa ishara ya ukombozi, ushindi, tumaini, Amani n.k 

Ni miaka elfu mbili sasa tokea Mwokozi wetu Yesu Kristo kufa na kufufuka na kubadili maana ya msaraba. Zamani ilikuwa ni mshangao kwa mtu kuvaa msaraba, kutundika msaraba katika nyumba ya ibada, kuweka au kuchora msaraba nyumbani kwako au kwenye nguo maana ni kifaa cha kuua, leo hii ni sawa ukute mtu kavaa shingoni kiti cha umeme, au kachora picha ya kitanzi nyumbani kwake itashangaza maana ni vifaa vya kuua lakini Bwana Yesu ameugeuza msaraba kutoka huko.
Msaraba leo unaimbwa kama kimbilio la watu wenye kutafuta ukombozi, amani, tumaini, ushindi, mwongozo, uponyaji n.k Lakini laity tukikumbuka kuwa msaraba ulikuwa ni kifaa cha kuua hakika ni vigumu kukimbilia kitanzi, sumu, upanga, kiti cha umeme, bunduki kama unatafuta tumaini, amani, furaha, wokovu maana haviwezi kufanya hivyo lakini msaraba ulibadilishwa kutokana na nguvu ya kifo cha Yesu.

KILA MTU ANAO MSARABA WAKE
Askari wa Kirumi wakiwa wametundika miili ya watu kwenye
misaraba pembezoni mwa njia.
Kila mtu anao msaraba wake na Yesu alisema mtu ambaye anataka kumfuta anatakiwa kubeba msaraba wake na kumfuata kila aendapo, je Bwana Yesu alikuwa na maana gani alipotuambia tubebe misaraba yetu na kumfuata?

Msaraba ni shida, matatizo, kama vile magonjwa, dhiki, umaskini, kukataliwa n.k Wengi tuna misaraba mingi katika maisha. Misaraba ni vile vitu au mambo ambayo yanatupa mateso na aibu mambo ambayo yanataka kutua yapo na unayo lakini Yesu anakuambia yabebe na umfuate nayo.

Kama Bwana Yesu aliweza kubadili msaraba wa aibu, mateso, uzuni na mauti kuwa tumaini, ukombozi, ushindi basi anaweza kubadili na msaraba wako huo wa utasa, umaskini, ugonjwa, talaka, kuachwa, kutoa kuolewa, kushindwa masomo, kukataliwa na ndugu na jamaa, kufilisika na kufanya kuwa ushindi, furaha, kichekona tumaini hakika anaweza kufanya na atafanya, alifanya kwa Ayubu mtu ambaye alizungukwa na misaraba mingi kama kufiwa na watoto wote, kufilisika, kupoteza mashamba na mifugo na kuumwa sana hakika Ayubu alibeba misaraba yake na kumfuata Mungu bila kukata tamaa na mwisho kila ambacho alikuwa amepoteza aliweza kurudisha mara mbili kitu ambacho labda hapo mwanzo hasingeweza lakini alipokubali kubeba misaraba yake na kumfuata Mungu iliwezekana.

Hata Yusufu, alipatwa na shida, taabu, kuonewa, kusingiziwa lakini aliweza kuibeba misaraba yake na kumfuata Mungu, hakika hakumwacha Mungu na mwisho wa siku kuuzwa kwake utumwani na ndugu zake kulikuwa ni njia ya kumpeleka Misri na kusingiziwa kwakwe na mke wa bosi wake na kupelekwa gerezani kulikuwa ndiyo njia ya kumpeleka kwa mfalme.

KUBEBA MSARABA NI NINI?
Kubeba msaraba ni kule kubaini shida na taabu ambazo unazo na kusimama imara zisije kuingilia Imani yako kwa Mungu kwa namna yeyote na kukutenga na Mungu kwa hali yeyote. Kubeba msaraba ni kule kuelewa hali uliyonayo na kusimama kwenye maombi kushindana mpaka mwisho, ni kule kumwita Mungu ndani ya uzuni na kilio chako. Unapopatwa na matatizo usiwaze kuwa utaangamia waza kuwa ni njia ya ukombozi, baraka na ushindi. Matatizo uliyonayo siyo kipimo cha maisha yako, usitazame tatizo na kusema sitaweza kuishi mda mrefu, usitazame tatizo na kusema nimekwisha au kusema basi, tazama tatizo kama njia ya kuendea baraka, kumkaribia Mungu, kumjua Mungu.

MATATIZO UJA ILI TUMJUWE MUNGU
Tunaposoma Biblia tunaweza kumjua Mungu alivyo na uwezo wake kutokana na matatizo waliyopata watu wake kwa mfano “Mungu anaweza kuokoa” tukisoma kitabu cha Danieli tunaona jinsi Danieli alivyotupwa katika shimo la simba lakini akataoka salama, pia juu Shedraki, Meshaki na Abedinego walivyotupwa katika tanuru la moto na kutoka hai, hakika tunajifunza Mungu anaokoa pia kwa wana wa Israeli walipokuwa Misri tunajifunza Mungu anaweza kumtoa mtu kwenye utumwa, utumwa wa umaskini, magonjwa, mapepo kama alivyowatoa utumwani kwa Farao n ahata alipojaribu kuwaangamiza aliweza kuangamia yeye na jeshi lake.

Ukubwa wa Mungu tunaujua tunaposoma kuwa aligawa bahari, alisimamisha jua wakati wa vita, alishusha mawe wakati Israeli ikipigana na adui zao na mengine mengi.

Hivyo misaraba uliyonayo pia ni darasa ambalo Mungu anataka ujifunze kuhusu yeye, usikubali msaraba ulionao kuwa ishara ya kifo, aibu, uzuni kwako bali simama imara na Mungu ataugeuza kuwa amani, ushindi na furaha.

Mwl. Judicate Fredy 
0765544589
0623655889

judicatemnyone@gmail.com

No comments:

Post a Comment