Sunday, 24 July 2016

JINSI YA KUKUZA UHUSIANO WAKO NA ROHO MTAKATIFU (SEHEMU YA 2)


Waandishi wa Agano jipya kamwe hawakusitasita kuheshimu na kuiinua nafsi ya tatu ya utatu mtakatifu (trinity), na wamekuwa wakirudia kusisitiza umuhimu wa kuishi ukiwa na uhusiano naye. Kasehemu moja, Yesu anawaambia wanafunzi wake kuwa ni kwa ajili yao na faida yao kuwa yeye awaache na kurudi mbinguni ili kwamba aweze kuwatumia Roho Mtakatifu (Taz Yohana 16:7). Hakika hii gharama na kujitoa kwa ajabu kwa umuhimu wa huduma ya Roho! Yesu kwa kusema hivyo alikuwa akimaanisha kwamba ni bora kuwa na Roho Mtakatifu  kuliko kuwa na mwana wa Mungu katika mwili (personal)! Yesu alibidi kuondoka ili Roho Mtakatifu aweze kuja, kwa maneno mengine tena ni kuwa ilibidi Yesu kujitenga na wanafunzi wake mwilini ili Roho Mtakatifu aje, kuwa na Yesu mwili siyo bora kuliko kuwa na Roho Mtakatifu.

Roho Mtakatifu anahitaji kuwa karibu na wewe katika maisha
yako.

Wednesday, 8 June 2016

JINSI YA KUKUZA UHUSIANO WAKO NA ROHO MTAKATIFU (SEHEMU YA 1)

 
 
Na Mwl Judicate Fredy

Roho Mtakatifu yupo kwa watu wote wa mataifa walio
mwamini Bwana Yesu na kumpa maisha yao.
Nchini Marekali palitokea na mzee mmoja katika jimbo la Califonia ambaye alikuwa anaishi kwenye kachumba kadogo kalichojaa takataka, mzee huyu alikuwa akipita mitaani na kuokota takataka katika mapipa ya takataka kwa muda wa miaka kumi na watu wengi walimzoea, alikuwa ni mkimya sana asiyeongea na mtu lakini ilitokea siku hakuonekana kwa muda wa siku mbili na jirani yake alishangaa maana mzee yule alikuwa kila siku akibeba takataka kutokana katika pipa lake la takataka lakini kwa siku mbili hakumwona na takataka zilikuwa nyingi ndipo alipoenda kugonga kwake kwa muda mrefu bila majibu ndipo alipoamuwa kuingia ndani ya chumba chake na kukuta mwili wa mzee yule ukiwa sakafuni, polisi walipokuja waligundua mzee yule alikufa kwa njaa na baridi lakini cha kushangaza pembeni yake kulikuwa na sanduku ambalo alikuwa ameshikili na kufa likiwa mkononi ndipo polisi walipofungua na kukuta noti ya dola moja, saa aina ya Rolex ya dola 500 na box
la plastiki ambalo ndani yake kulikuwa na cheni za dhahabu na pete zenye almasi ambazo zen
ye thamani sawa na dola zaidi ya 22000, jambo hili liliweza kushangaza watu kuwa iliwezekana

Saturday, 14 May 2016

USHAURI NA MAOMBEZI

 
Wasiliana nami Mwl Judicate Fredy kwa:
 
Namba ya simu +255 765 544 589
             E-mail www.judicatemnyone@gmail.com
                                                      Facebook judicate_fredy

Natumaini kusikia kitu kwako, ukiwa na maswali juu ya kitu chochote kuhusu Neno la Mungu na maisha nitafute kwa mawasiliano hayo.

IJUE SIRI YA BOYFRIEND NA GIRLFRIEND 4

 
MAANA ILIYOFICHIKA YA GIRLFRIEND NA BOYFRIEND

Nataka ujue maana ya girlfriend na boyfriend, kama jinsi Shetani anavyoitumia, na jinsi anavyochochea tafsiri yake ndani ya watu wengi na kuwaangusha katika zinaa (dhambi)

Kwa maana ya ndani iliyofichwa na kufunikwa kwa maneno mazuri yaani girlfriend na boyfriend, ni hii; Ni uhusiano wakaribu sana kati ya watu wa jinsi tofauti na mara nyingi huambatana na kufanya ngono (zinaa)

Vijana wengi hawaukubali ukweli huu, na ndiyo maana nikakuuliza unapata hisia gani unaposema girlfriend au boyfriend wangu, tofauti na uposema rafiki yangu kwa hali ya kawaida? Kama na wewe unaipinga maana hiyo niliyokuambia fanya hivi; Jaribu kumuuliza msichana mwenye akili timamu kama anaye girlfriend, au muulize mvulana ambaye ni rafiki yako akuambie kama anaye boyfriend. Nina uhakika hatakupa jibu la moja kwa moja na ukipigwa usishangae, na usiseme Mwalimu Judicate amenituma.




"Mchumba ni mtu wa jinsia tofauti na wewe ambaye umemposa
 au umeposwa naye na tena umefanya naye shauri au
 patano au mkataba au agano kuwa utaoana naye".


    Vijana wengi hupenda kuwa na girlfriend au boyfriend wakiwa na maana ya urafiki wa kawaida, wakipendana, wakisaidiana na kushirikiana mambo mbalimbali mazuri.

Saturday, 30 April 2016

IJUE SIRI YA GIRLFRIEND NA BOYFRIEND-3



MAPENZI

Mapenzi ni kitu kilichowekwa na Mungu ndani ya kila mwanadamu. Mapenzi ni kitu kilicholala na huamka yenyewe kwa wakati ambao Mungu amepanga kwa kila mtu. Hivyo mapenzi yapo ndani ya kila mtu tangu anapozaliwa, ila huwa yamelala, na yana muda wake wa kuamka.

“Nawasihi enyi binti za Yerusalemu,… msiyachochee mapenzi wala kuyaamsha, hata yatakapoona vema yenyewe”
(Wimbo 2 :7)


Ni wale tu wenye kwenda na muda na majira ufikia ndoto zao
            Utakubaliana nami kuwa huwezi kuamsha kitu ambacho hakijalala, kwa hiyo mapenzi huwa yamelala. Anaposema ‘yatakapoona vema yenyewe’ maana yake Mungu alikwisha yapangia utaratibu na muda wake ili yaamke. Kumbuka kila kitu alichokifanya Mungu ni kizuri na chema hivyo alijua hali halisi ya ujana, hali yetu ya kibayolojia ndiyo maana akaweka muda wa mapenzi kuamka. Biblia inasema mapenzi huweza kuamshwa na mtu mwenyewe.


“…enyi binti za Yerusalemu,…msiyachochee mapenzi wa
la kuyaamsha…”

(Wimbo 2 :7)

Sunday, 14 February 2016


ETI YESU NI VALENTINE WAKO?? HIVI UNAJUA UNALOSEMA??


Picha ya aitwaye Valentine aliyekuwa
Inakaribia February 14, huitwa siku ya Wapendano. Unaulizwa maswali na watu, je, mtu aliyeokoka anaweza kushiriki Valentine day? Hili kwangu linaweza kuwa swali gumu sana. Inawezekana wapo watumishi waliowahi kujibu kwamba Wakristo hawapaswi kushiriki kwa sababu hii sio ya Kikristo, kwangu inaweza kuwa ngumu kidogo kutumia kigezo kwamba sio ya Kikristo hivyo watu wasijihusishe nayo.

Maana kama kigezo ni hicho tu kwamba sio ya Kikristo, swali moja najiuliza; hapa Tanzania tuna sherehe za Muungano, Uhuru na Mapinduzi, tuna zingine kama MEI MOSI, na zinginezo ikiwemo NYERERE DAY, sioni kama hizo ni za Kikristo, lakini mbona wanashiriki?
Mimi nadhani kuna haja ya kurudi nyuma na kuchunguza historia ya namna hii siku ilianzishwa, na nini malengo yake ya kuadhimishwa. Mimi nilijipa muda huo tangu siku za nyuma, nimekuwa nikieleza maoni yangu sio leo tu, na hapa nitaeleza tena kidogo.

Sunday, 7 February 2016

IJUE SIRI YA GIRLFRIEND NA BOYFRIEND -2


UPENDO NI NINI?
Mara nyingi vijana hudanganyana kwa kuambiana nakupenda lakini hawajui nini maana halisi ya upendo au wakati mwingine wanakuwa na upendo wa kinafiki. Upendo ni hali ya ndani ya moyo au nafsi na huelezwa kwa maneno na kwa matendo makuu mazuri yafanywayo kutoka ndani ya moyo. Upendo hauangalii gharama za kufanya tendo la upendo. 
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele”(Yohana 3:16)