Monday, 12 September 2016

MAMBO AMBAYO YANAWAHANGAISHA WATU

: Mwana wa Mungu lazima uvuke hapa!
(Chakula, Vinywaji, Mavazi na kesho)



Mathayo 6:25-34

25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

 26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

 27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

Saturday, 10 September 2016

JINSI YA KUTUNZA NDOTO YAKO ILI IWEZE KUTIMIA


Tunaposoma Biblia tunaona Mungu mara nyingi akisema na watu kupitia ndoto wawapo wamelala kama vile Ibrahimu, Yakobo, Yusufu, Suleimani, Yusufu (baba wa Yesu), Petro n.k  Na bado mpaka leo Mungu anaendelea kusema na watu kupitia ndoto lakini baadhi ya watu upuuza ndoto kwa kkuto kujua ndoto ni kitu gani katika maisha ya kiroho.
Kimsingi ndoto ni picha za matukio

1. KUSHIKA SHERIA ZA MUNGU

Sheria za Mungu ni Neno lake, ili uweze kutunza ndoto yako na kuifanya itimie sawa na Mungu alivyopanga na wakati usika ni vizuri kusoma Neno la Mungu na kulitimiza kama lisemavyo. Unapoona umeenda nje ya Neno la Mungu na kutenda dhambi geuka mara moja na utubu na kumwomba Mungu akaupe nguvu za kushika sharia yake na songambele.

Ndoto ni kama mshumaa uwakao, unahitaji kutunzwa usije
kuzimwa na upepo uvumao wa adui Shetani na wakala wake.
2. KUISHI MAISHA YA MAOMBI

Watu wengine kwa kuwa wanajua ndoto ni bayana na hakika zitokee hivyo wakiota tu ndoto uacha kuomba na kusema zitatokea bila kujua maombi pia uhitajika kutengeneza njia ya kuelekea kwenye ndoto yako kwa mda usika. Lazima kama mkristo kishi maisha ya kushindana na kujua wakati wote kunapotokea jambo la kimungu basi Shetani naye ujiinua hivyo unapoota ndoto njema ya kimungu tambua Shetani naye anajiandaa kuzuia isitokee hivyo kaa katika maombi daima mpaka iweze kutimia.