Saturday, 30 April 2016

IJUE SIRI YA GIRLFRIEND NA BOYFRIEND-3



MAPENZI

Mapenzi ni kitu kilichowekwa na Mungu ndani ya kila mwanadamu. Mapenzi ni kitu kilicholala na huamka yenyewe kwa wakati ambao Mungu amepanga kwa kila mtu. Hivyo mapenzi yapo ndani ya kila mtu tangu anapozaliwa, ila huwa yamelala, na yana muda wake wa kuamka.

“Nawasihi enyi binti za Yerusalemu,… msiyachochee mapenzi wala kuyaamsha, hata yatakapoona vema yenyewe”
(Wimbo 2 :7)


Ni wale tu wenye kwenda na muda na majira ufikia ndoto zao
            Utakubaliana nami kuwa huwezi kuamsha kitu ambacho hakijalala, kwa hiyo mapenzi huwa yamelala. Anaposema ‘yatakapoona vema yenyewe’ maana yake Mungu alikwisha yapangia utaratibu na muda wake ili yaamke. Kumbuka kila kitu alichokifanya Mungu ni kizuri na chema hivyo alijua hali halisi ya ujana, hali yetu ya kibayolojia ndiyo maana akaweka muda wa mapenzi kuamka. Biblia inasema mapenzi huweza kuamshwa na mtu mwenyewe.


“…enyi binti za Yerusalemu,…msiyachochee mapenzi wa
la kuyaamsha…”

(Wimbo 2 :7)