MAPENZI
Mapenzi ni kitu kilichowekwa na Mungu ndani ya kila
mwanadamu. Mapenzi ni kitu kilicholala na huamka yenyewe kwa wakati ambao Mungu
amepanga kwa kila mtu. Hivyo mapenzi yapo ndani ya kila mtu tangu anapozaliwa,
ila huwa yamelala, na yana muda wake wa kuamka.
“Nawasihi enyi binti za
Yerusalemu,… msiyachochee mapenzi wala kuyaamsha, hata yatakapoona vema
yenyewe”
(Wimbo 2 :7)
Utakubaliana nami kuwa huwezi kuamsha
kitu ambacho hakijalala, kwa hiyo mapenzi huwa yamelala. Anaposema ‘yatakapoona
vema yenyewe’ maana yake Mungu alikwisha yapangia utaratibu na muda wake ili
yaamke. Kumbuka kila kitu alichokifanya Mungu ni kizuri na chema hivyo alijua hali
halisi ya ujana, hali yetu ya kibayolojia ndiyo maana akaweka muda wa mapenzi
kuamka. Biblia inasema mapenzi huweza kuamshwa na mtu mwenyewe.
![]() |
Ni wale tu wenye kwenda na muda na majira ufikia ndoto zao |
“…enyi binti za Yerusalemu,…msiyachochee mapenzi wa
la kuyaamsha…”
(Wimbo 2 :7)