Sunday, 14 February 2016


ETI YESU NI VALENTINE WAKO?? HIVI UNAJUA UNALOSEMA??


Picha ya aitwaye Valentine aliyekuwa
Inakaribia February 14, huitwa siku ya Wapendano. Unaulizwa maswali na watu, je, mtu aliyeokoka anaweza kushiriki Valentine day? Hili kwangu linaweza kuwa swali gumu sana. Inawezekana wapo watumishi waliowahi kujibu kwamba Wakristo hawapaswi kushiriki kwa sababu hii sio ya Kikristo, kwangu inaweza kuwa ngumu kidogo kutumia kigezo kwamba sio ya Kikristo hivyo watu wasijihusishe nayo.

Maana kama kigezo ni hicho tu kwamba sio ya Kikristo, swali moja najiuliza; hapa Tanzania tuna sherehe za Muungano, Uhuru na Mapinduzi, tuna zingine kama MEI MOSI, na zinginezo ikiwemo NYERERE DAY, sioni kama hizo ni za Kikristo, lakini mbona wanashiriki?
Mimi nadhani kuna haja ya kurudi nyuma na kuchunguza historia ya namna hii siku ilianzishwa, na nini malengo yake ya kuadhimishwa. Mimi nilijipa muda huo tangu siku za nyuma, nimekuwa nikieleza maoni yangu sio leo tu, na hapa nitaeleza tena kidogo.

Sunday, 7 February 2016

IJUE SIRI YA GIRLFRIEND NA BOYFRIEND -2


UPENDO NI NINI?
Mara nyingi vijana hudanganyana kwa kuambiana nakupenda lakini hawajui nini maana halisi ya upendo au wakati mwingine wanakuwa na upendo wa kinafiki. Upendo ni hali ya ndani ya moyo au nafsi na huelezwa kwa maneno na kwa matendo makuu mazuri yafanywayo kutoka ndani ya moyo. Upendo hauangalii gharama za kufanya tendo la upendo. 
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele”(Yohana 3:16)